Hazina-Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar

Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wataalamu wa Udhibiti wa Ubadhirifu na Ufisadi Tanzania ( ACFE) leo tarehe 27/01/2025 wametia saini hati ya mashirikiano (MoU)Mafunzo haya kwa Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma yameandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina yakilenga kuwajengea uwezo zaidi

January 27, 2025

Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wataalamu wa Udhibiti wa Ubadhirifu na Ufisadi Tanzania ( ACFE) leo tarehe 27/01/2025 wametia saini hati ya mashirikiano (MoU) yenye lengo la kushirikiana katika maeneo yafuatayo:

  1. Kutoa elimu kwa watendaji wa taasisi za umma katika kujua masuala ya ubadhirifu na ufisadi unaofanyika katika taasisi za umma.
  2. Kutoa elimu ya masuala ya kubaini, kugundua na kujiepusha na ubadhirifu na ufisadi katika mashirika ya umma.
  3. Kuwa na mashirikiano ya karibu katika masuala ya ukaguzi maalum na uchunguzi wa vihatarishi mbali mbali katika mashirika ya umma.
  4. kuanza kuwajengea uwezo maafisa wa ofisi ya Msajili Wa Hazina Zanzibar.
  5. Kushiriki mikutano na mafunzo ya kikanda na kimataifa kwa maafisa wa ofisi ya Msajili Wa Hazina
    Mashirikiano hayo yatakuwa kwa muda wa miaka 3 na kutakuwa na kamati ya wataalamu kutoka pande zote mbili ili kusimamia na kuyafanyia kazi maeneo ya mashirikiano