Kwa niaba ya Msajili wa Hazina, Ndugu Khadija Masoud Haji Mkurugenzi Utumishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina akipokea Tunzo ya shukrani kutoka kwa Uongozi wa Taasisi ya Wataalamu wa Udhibiti wa Udanganyifu katika Kongamano la Kimataifa la Mapambano dhidi ya Udanganyifu katika Nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki.

Kwa niaba ya Msajili wa Hazina, Ndugu Khadija Masoud Haji Mkurugenzi Utumishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina akipokea Tunzo ya shukrani kutoka kwa Uongozi wa Taasisi ya Wataalamu wa Udhibiti wa Udanganyifu katika Kongamano la Kimataifa la Mapambano dhidi ya Udanganyifu katika Nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki. Kongamano hilo limeanza Tarehe 24-28 Februari, 2025 katika Ukumbi wa Madinat Al Barah Zanzibar.
Mkufunzi wa Warsha ya kuwajengea uwezo Wahasibu Wakuu wa Taasisi za Uwekezaji wa Umma kutoka Shirika la Kimataifa la Fedha (IMF).

Mkufunzi wa Warsha ya kuwajengea uwezo Wahasibu Wakuu wa Taasisi za Uwekezaji wa Umma Ndugu Dzingai F. Chaptuwa kutoka Shirika la Kimataifa la Fedha (IMF). Warsha hiyo imeanza Tarehe 24-28 February, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi za ZAWA Zanzibar.
Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar inashajihisha Mashirika ya Uwekezaji kuwekeza katika Hati fungani (SUKUU)

Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar inashajihisha Mashirika ya Uwekezaji kuwekeza katika Hati fungani (SUKUU) inayofuata miongozo ya shariah za kiislam na kuekeza katika Miradi ya kimaendeleo Zanzibar na kupata faida mara mbili kwa mwaka . wekeza sasa kwa maendeleo ya Zanzibar
“Azma ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi ni kuleta mabadiliko kwa mashirika na taasisi za umma Zanzibar”-Mhe Dkt. Saada Salum Mkuya

“Azma ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi ni kuleta mabadiliko kwa mashirika na taasisi za umma Zanzibar. Kumekuwa na mabadiliko makubwa ya kimaendeleo kwenye Mashirika ya Umma hususan katika kutoa huduma bora kwa wananchi, kuhakikisha yanakamilisha malengo na mikakati ya Serikali iliyojiwekea.” Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na MipangoMhe Dkt. Saada Salum Mkuya
Serikali imeanzisha mashirika na taasisi za umma ili kupata ufanisi katika sekta mbalimbali na ziweze kuchangia mapato ya kuendesha shughui za Serikali na kupatikana fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo na sio kuwa mzigo kwa taifa, yaani sio kufanya shughuli zake kwa hasara.

Serikali imeanzisha mashirika na taasisi za umma ili kupata ufanisi katika sekta mbalimbali na ziweze kuchangia mapato ya kuendesha shughui za Serikali na kupatikana fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo na sio kuwa mzigo kwa taifa, yaani sio kufanya shughuli zake kwa hasara.
Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wataalamu wa Udhibiti wa Ubadhirifu na Ufisadi Tanzania ( ACFE) leo tarehe 27/01/2025 wametia saini hati ya mashirikiano (MoU)Mafunzo haya kwa Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma yameandaliwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina yakilenga kuwajengea uwezo zaidi

Msajili wa Hazina kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wataalamu wa Udhibiti wa Ubadhirifu na Ufisadi Tanzania ( ACFE) leo tarehe 27/01/2025 wametia saini hati ya mashirikiano (MoU) yenye lengo la kushirikiana katika maeneo yafuatayo:
Msajili wa Hazina Sanya abainisha mafanikio ikiwemo kupanda kwa gawio laserikali, asisitiza dhamira na malengo ya Rais Dk. Mwinyi lazima yatimizwe

Uwepo wa Mashirika ya Umma ni kichocheo cha maendeleo ya Uchumi”. Hii ni kauli mbiu inayotumiwa na Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar kuonyeshaumuhimu wa mashirika na taasisi za umma katika maendeleo ya nchi.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amekuwa mstari wa mbele kuchagiza mafanikio makubwa ya mashirika na taasisi za umma kutokana na maono yake.Ofisi ya Msajili wa Hazina Zanzibar inayoongozwa na Waheed Ibrahim Muhammed Sanya imemtaja Dk. Mwinyi kuwa kielelezo cha mafanikio na utendaji wa mashirika na taasisi za umma ikiwemo kuongezeka kwa gawio la serikali kwa mashirika hayo kutoka sh. bilioni 5.8 hadi sh. bilioni 13.7.